Wednesday 8 March 2017

LUCIANA DANDA, MJAMZITO ALIYEKUWA AKIPOTEZA DAMU KILA MWEZI

Lusiana Danda (26) alipokuwa na Ujauzito wa miezi nane (Oktoba 2012), alikuwa anatokwa na damu ya mwezi.

Hali hii ambayo ni hatarishi kwa mjamzito na mimba yake ilianza ujauzito ukiwa na miezi minne, baada ya kuugua malaria. 

Lusiana, ambaye ni mkulima na mkazi wa kijiji cha Ifinga, Songea mkoani Ruvuma, alipata matibabu katika zahanati ya Ifinga.

Alivyokutwa na malaria, alipewa dozi ya dawa ya mseto ambayo hakuimaliza. “Niliamua kuacha kumeza dawa baada ya kusikia naendelea vema. Pia, nilipokuwa nameza dawa hizo nilikuwa nasikia maumivu chini ya kitovu; nikahofia mimba yangu isije kutoka,” alisema Lusiana.

Dada huyu hakuwa na mume na hakuwa na mahusiano na mwanaume aliyempa mimba aliyokuwa nayo wakati huu. 

Kwa kuwa tayari alikuwa na watoto wawili na pasipokuwa na mtu mwingine wa kumtegemea, Lusiana aliendelea na kazi za kulima kama kibarua bila ya kupumzika, japokuwa alikuwa mjamzito na anaumwa.

Anasema siku moja, Lusiana akiwa shambani na baada ya kulima kwa saa mbili, ghafla aliaanza kusikia maumivu makali chini ya kitovu.

Maumivu hayo yalikuwa yakizidi kadiri muda ulivyokwenda na alikuwa akijisikia hali ya kutaka kujisaidia haja ndogo.

Alipoenda msalani kujisaidia, ndipo akashtukia kuwa haukuwa mkojo bali ilikuwa ni damu. Damu hii iliendelea kutoka kidogokidogo kwa siku tatu bila kukatika, ndipo Lusiana aliamua kwenda zahanati ya Ifinga kupima kama ujauzito wake bado ulikuwa salama.

“Nilipofika zahanati niliambiwa nitoe Tsh. 2,000 ili nipimwe kujua kama mimba bado ipo. Nilikuwa sina pesa kwa hiyo nilirudi nyumbani nikiwa sina raha,” alisema Lusiana.

Japokuwa damu ilikoma kutoka siku hiyo hiyo ya tatu, baada ya wiki mbili, Lusiana alifanikiwa kupata Sh10, 000 na kurudi tena kwenye zahanati kufanya kipimo cha ujauzito.

Kipimo kilionesha kwamba bado alikuwa mjamzito lakini, mwezi uliofuata damu iliendelea kutoka tena na Lusiana aliporudi kwenye zahanati ya Ifinga kwaajili ya kujua kwa nini, hakufanikiwa.

“Niliambiwa hakuna vifaa vya kuchunguza kujua kama damu inayotoka inasababishwa na nini; na mhudumu wa afya aliniambia kuwa hajasomea kujua damu inayotoka kwa mjamzito inasababishwa na nini,” alisema Lusiana.

Kwa mujibu wa Dk. Ahmed Makuani, mtaalam wa magonjwa ya wanawake na uzazi salama kutoka Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, kutokwa na damu kwa mjamzito ni kiashirio cha hatari sana.

Mjamzito akiona damu inatoka anatakiwa kuwahi haraka hospitali. Dk. Makuani alisema wanawake walio na umri wa zaidi ya miaka 35 wakishika mimba wako katika hatari ya kupoteza damu kwa sababu ya kondo la nyuma kuning’inia katika shingo ya kizazi upande wa ndani.

Tatizo hili linajulikana kama placenta previa. Kitendo cha kondo la nyuma kuvumba kinaweza kusababisha kuachia sehemu iliyojishika na kutoa damu sehemu ile iliyoachia, pamoja na kuziba njia ya uzazi kuwa ndogo na mtoto kushindwa kutoka vizuri, kuzaliwa mtoto mfuu kwa kukandamizwa na kondo hilo, kuzaliwa mtoto njiti pamoja na kuzaliwa mtoto mwenye uzito mdogo.

Naye aliyekuwa Naibu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Dk. Seif Rashid anasema kuwa tatizo la mjamzito kupoteza damu ni tatizo sugu na kubwa sana hapa nchini Tanzania na ndio chanzo kikubwa cha wajawazito kufariki.

Dk. Rashid alisema kuwa, wataalam wa kulitatua tatizo hilo wapo wachache sana katika zahanati mbalimbali za vijijini ambako asilimia 75 ya watanzania ndio wanaishi huko.

“Kwa sasa tupo katika mkakati wa kuboresha zahanati mbalimbali kwa kuwapeleka watumishi wa sekta ya afya kusoma, masuala ya uuguzi kwa miaka miwili ili muuguzi anapokutana na tatizo hilo awe na ujuzi wa kumsaidia mjamzito,”alisema Dk. Rashid.

Wakati Sera ya Afya ya 2007 inasistiza utoaji wa huduma bora na bure kwa mjamzito, hili bado ni changamoto kwa maeneo kama Ifinga, Songea.

Zahanati ya Ifinga ina nesi mmoja na muhudumu wa afya aliyefika darasa la saba mmoja. Pia, katika zahanati hiyo, kuna mganga moja na mpimaji magonjwa maabara mmoja.

Hakuna mtaalam wa magonjwa ya mjamzito na wala hakuna vifaa tiba kama mashine ya kumsaidia mtoto kupumua akizaliwa.

Kwa wakati huu, ambapo Lusiana alikuwa ni mjamzito na kuhitaji huduma hizi, kulikuwa hakuna dawa za kumchoma sindano mama ili mfuko wa uzazi usinyae baada ya kujifungua na mzani wa kupimia mtoto akizaliwa mbovu.

Japokuwa ameshindwa kupata ufumbuzi wa tatizo lake, Lusiana anatarajia kujifungua katika zahanati ya Ifinga. Hana uwezo wa kwenda katika hospitali ya Peramiho inayomilikiwa na Kanisa Katoriki Jimbo la Ruvuma, ambapo ni kilometa 243 kutoka katika kijiji cha ifinga.

Nauli ya kwenda ni Tsh.38,000 na gharama za kujifungua ni Tsh. 11,000; hapo bado gharama za kuishi. Kaimu Mganga Mkuu wa Wilaya ya Songea Dk. Daniel Masawe alisema kuwa katika wilaya hiyo, wajawazito 95 kati ya 100,000 kila mwaka wanapoteza maisha kwa sababu ya upungufu wa damu.

Alithibitisha kwamba vifo hivi vinachangiwa na ukosefu wa vifaa tiba pamoja na wataalam wa kumsaidia mjamzito kujifungua salama katika zahanati mbalimbali kwenye wilaya hiyo. "Kwa sasa watalaam wa kumsaidia mjamzito kujifungua salama ambao wamebobea katika ukunga hapa Songea ni wanne tu, ukilinganisha na zahanati 35 tulizonazo," alisema Dk. Masawe.

 Mtaalam wa magonjwa ya akinamama katika hospitali ya Peramiho Dk. Marieta Mtumbuka alisema kuwa mwezi Septemba mwaka 2012, wajawazito wawili walifika katika hospitali hiyo wakiwa na tatizo la kupoteza damu.

Kati ya hao ni mmoja alikuwa na miaka 37. Mjamzito akiumwa malaria na kucheleweshwa au kutokumaliza matibabu, anakuwa hatarini kupatwa na tatizo la kutokwa na damu.

Ndiyo maana, kwa mujibu wa Dk. Rashid kuna umuhimu wa mjamzito kutumia dawa ya mseto kwa sababu ndio dawa pekee iliyofanyiwa utafiti na kugundulika inaweza kutibu na kumkinga mjamzito na mtoto aliye tumboni na malaria akitumia kipindi ambacho haumwi malaria.

“Wizara imeamua kupitisha dawa ya mseto baada ya tafiti mbalimbali kubaini dawa ya chloroquin inausugu wa kuzoeleka na wadudu wa malaria. Tulipotoka katika dawa ya chloroquin tukaanza matumizi ya dawa ya fansider lakini nayo ikaonesha uwezo mdogo wa kukabiliana na wadudu wa malaria.

Baada ya utafiti ndio tumegundua dawa mbadala ya kumkinga mjamzito na malaria ni dawa mseto,” alisema na kuongeza kuwa mjamzito anapewa dawa ya mseto akiwa na mimba ya wiki 20 na wiki ya 28.

Katika kitabu cha hotuba ya makadilio ya mapato na matumizi ya mwaka wa fedha 2012/2013, kinafafanua kuwa jumla ya dozi 9,196,080 za dawa mseto pamoja na kusambaza vyandarua vya hati punguzo vyenye viuatilifu 5,412579 kwa wanawake wajawazito lakini Lusiana hana chandarua.

"Nilipoanza kwenda zahanati kupima ujauzito wangu, sikupewa chandarua. Niliambiwa vimekwisha na sina uwezo wa kununua chandarua hivyo nalala bila ya kutumia hicho chandarua,"alisema Lusiana.

Aidha kwa mujibu wa bajeti ya afya ya mwaka 2012/2013, kumekuwa na ongezeko la vituo vya afya na zahanati za serikali na binafsi, kuanzia mwaka 2005 kutoka zahanati 4,322 hadi zahanati zahanati 4,679 mwaka 2012.

wa upande wa vituo vya afya, kumekuwa na ongezeko kutoka 481 mwaka 2006 hadi kufikia 742 mwaka 2012 na kwa upande wa hospitali kutoka 219 hadi kufikia 241.

Bado kuna wanawake kama Lusiana wanaoshindwa kupata huduma za afya zenye ubora na kwa gharama wanazoweza kuzimudu.

Source; Gordon Kalulunga

Tuesday 5 July 2016

TACOMO KWA KUSHIRIKIANA NA WOMEN FUND TANZANIA WATOA MAFUNZO YA UONGOZI NA HAKI KWA WANAWAKE NA WASICHANA WANAOFANYA BIASHARA KATIKA MASOKO MPANDA MKOANI KATAVI

SERA ya maendeleo ya wanawake na jinsia ya mwaka 2000 ni moja wapo ya miongozo ya serikali katika jitihada za kuwapa wananchi mwelekeo wa Maendeleo ya wanawake na jinsia utakaohakikisha kuwa sera, Mipango, Mikakati na shughuli mbalimbali za maendeleo katika kila sekta na taasisi katika  ngazi zote zinazingatia usawa wa jinsia.

Sera hiyo inachukuwa nafasi ya sera ya Wanawake katika maendeleo ya mwaka 1992 ili kuingiza dhana ya jinsia katika maendeleo ya jamii.

Dhana  ya jinsia ni mtazamo mpya wa kuharakisha maendeleo kwa
kuangalia mahusiano ya jamii kati ya wanawake na wanaume ambayo yanatambua tofauti zilizopo za kijinsi (sex) baina yao pamoja na mgawanyo wa majukumu katika jamii.

Ili kuweza kupata maendeleo ya haraka na endelevu dhana ya jinsia pia inatilia mkazo umuhimu wa kushirikiana na kufanya kazi kwa kutegemeana kati ya wanawake na wanaume.

Hii inatokana na ukweli kuwa, majukumu ya wanawake katika jamiini tofauti nay ale ya wanaume na kuwa yote ni muhimu kwa maendeleo ya familia, jamii na Taifa.

Mwelekeo wa maendeleo ki-jamii, kitaifa na ki-mataifa hivi sasa
unasisitiza na kuhimiza upangaji na utekelezwaji mipango unaozingatia ushirikishwaji wa wanawake na wanaume kwa pamoja katika kutambua, kuthamini na kukuza vizuri zaidi uwezo wa wananchi katika kujiletea maendeleoyao.

Utekelezaji wa sera hiyo unazingatia mchango wa sekta mbalimbaliu za serikali na zisizo za serikali, wataalam mbalimbali wakiwemo wasomi na wanataaluma na watu binafsi wanawake na wanaume. Msukumo upo kwenye kuingiza masuala ya jinsia (Gender Mainstreaming) na kuhakikisha kuwepo kwa shughuli mbalimbali zinazowalenga wanawake (Woman Specific)
ili kuharakisha kuwepo usawa wa kijinsia unaotarajia.

Kutokana na sera hiyo kuelezea pia kuhusu mashirika yasiyo ya
kiserikali kuhusika katika utekelezaji wa sera ya maendeleo ya
wanawake na jinsia, shirila lisilo la kiserikali la Tanzania Community Media Organization(TACOMO), limetoa mafunzo ya kukuza sauti na kuwaimarisha haki za wanawake na wasichana kushiriki nafasi za uongozi katika maeneo ya Masoko ya Manispaa ya Mpanda mkoani Katavi, chini ya ufadhili wa Woman Fund Tanzania.
Mafunzo hayo ya siku mbili, yalifanyika katika ukumbi wa Shule ya
Sekondari ya St. Mary’s ya Kashaulili huku wanawake 80 na wanaume 11wakishiriki katika mafunzo hayo na mdahalo.

Mkurugenzi wa shirika hilo, Gordon Kalulunga ambaye pia ni Mwandishi wa habari aliyebobea katika nyanja za habari za Afya ya uzazi na dawa za kulevya nchini, aliwataka wanawake na wasichana waliokuwa wameshiriki katika mafunzo hayo, kuwa majasiri na kushiriki katika kuwania nafasi za uongozi ili kuweza kupaza sauti zao.

“Shime natoa kwenu, jitokezeni katika kuwania nafasi za uongozi katika nyanja zote kuanzia huko sokoni, mahala mnapoishi na wale ambao wana vyama vya siasa pia jitokezeni na anapojitokeza mwanamke wanawake wengine muungeni mkono kwa kumchagua”alisema Kalulunga.

Aidha alisema kuwa kuna changamoto kubwa ambao anaiona kwa wanawake wengi kuwa ni uwoga ambao unatokana na viongozi wa serikali hasa ngazi za mitaa, Vijiji na wilaya kutowajulisha wananchi majukumu yao kama viongozi hivyo wananchi hasa wanawake wanabaki katika kifungo cha woga hata wa kuhoji wakihofia misukosuko ya viongozi wa serikali wasio waadilifu.

Wakati anayasema hayo, Ofisa Maendeleo ya jamii wa kata ya Kashaulili na majengo ambaye pia alikuwa mwezeshaji, Imelda Mkama, alipotakiwa kuwaeleza washiriki wa mafunzo hayo majukumu yake ili wafahamu na kuhamasika kuoimba ushauri kutokana na kazi zake, alikataa katu katu na kwamba atakutana nao siku nyingine.

Akitoa mada ya ujasiliamali na uongozi, Ofisa huyo aliwataka wanawake hao kuwa hodari katika kuthubutu.

“Wajasiliamali wengi si wabunifu bali wanaiga biashara. Tusiwe na
biashara moja maana ukimwezesha mwanamke mmoja, umewezesha watu 10.”Alisema Imelda.

Aidha alitoa elimu ya uundwaji wa vikundi kwa wanawake hao na
kuwaambia kuwa pesa ambazo zinatarajiwa kwenda kila kijiji maarufu kama Milioni 50 za Magufuli, hazitagawiwa kwa mtu mmoja mmoja bali zitakopeshwa kwenye vikundi ambavyo vimesajiliwa, hivyo kwa wale ambao wanahitaji kusajili vikundi na kuandika katiba, milango ipo wazi katika ofisi yake.

Katika masoko ya Buzogwe na Mapnda Hoteli, uchaguzi wa uongozi wa masoko hayo unatarajiwa kufanyika June 30, mwaka huu ambapo wanawake kadhaa wamehamasika kuwania nafasi mbalimbali huku wakisema kuwa wanahitaji zaidi elimu na mafunzo kama yaliyotolewa na shirika la TACOMO.

Mwenyekiti wa Soko la Mpandfa Hotel, Boniface Mganyas, ambaye ni mkazi wa Majengo, anasema kuwa wanawake wengi huko nyuma walikuwa na woga wa kujitokeza katika kuwania nafasi za uongozi lakini baada ya semina hiyo tayari wanawake wawili wamejitokeza kujaza fomu za uongozi.



 Naye Mwenyekiti wa soko la Buzogwe, Ramadhan Karata, anasema kumekuwa na changamoto kubwa kuwapata viongozi wanawake ambao baadhi wanazuiliwa na waume zao kuwania nafasi za uongozi.

“Mafunzo kama haya yakiendelezwa yatasaidia sana kuwaondoa wanawake uwoga wa kujitokeza kuwania nafasi za uongozi katika jamii maana wengi hawana elimu za kutosha ili hali wana hulka za uongozi, hivyo naomba TACOMO mrudi tena na tena na muende katika maeneo mengine kuwahamasiha wanawake ili waweze kujitokeza na pale kwenye soko letu mwanamke mmoja
amesema nimjazie fomu” alisema Karata.

Mkufunzi wa mada ya haki za wanawake, William Simwali, ambaye anaishi na ualubino, aliwataka wanawake hao kuondoa woga kujitokeza katika uongozi na kwamba wajifunze kwa wanawake wenzao ambao ni viuongozi katika Taifa hili na wote wanaweza.

Naye mshiriki wa mafunzo hayo Mwasiti Mohammed, alisema yeye kabla ya uchaguzi wa masoko hayo, atajitokeza pamoja na baadhi ya wanawake wenzake kwenda kuishamilisha elimu aliyoipata kutoka TACOMO na kwamba yeye pia mwaka 2017 atawania nafasi ya uongozi katika Chama Cha Mapinduzi (CCM).

“Wanawake wengi tunahitaji elimu kama hizi, hivyo naona kuna haja ya kuwafuata wanawake huko huko waliko na kutoa elimu hizi za uongozi za kukuza sauti na kuwaimarisha haki za wanawake na wasichana kushiriki nafasi za uongozi katika maeneo ya Masoko ya Manispaa ya Mpanda”alisema Mwasiti.

Monday 4 July 2016

Shisha yapigwa marufuku Tanzania, hakuna kuvuta sigara hadharani Dar


WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa, jana amemaliza kazi. Amepiga marufuku matumizi ya ulevi aina ya Shisha nchini ambao umesambaa kwa vijana wengi pamoja na watu wazima.

Marufuku yake imekuja siku chache baada ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda, kupiga marufuku matumizi ya kilevi hicho pamoja na uvutaji wa sigara hadharani mkoani humo.

Wengi, hata ambao hawakuwahi kutumia sigara maishani mwao, walikuwa wamekimbilia uvutaji wa Shisha kwa kujidanganya kwamba kilevi hicho ambacho nacho kinavutwa, hakina madhara kama sigara.

Wanawake kwa wanaume wanavuta Shisha, wengine hadharani, na huona fahari wanapojisikia kulewa huku wakijifariji kwamba hawawezi upata madhara.

Lakini marufuku ya Waziri Mkuu imemaliza kazi, kwa sababu hivi sasa kilevi hicho kimeharamishwa na hakina tofauti na dawa za kulevya.

Katazo la uvutaji wa sigara hadharani limewakumba wengi, kwani si mmoja au wawili wanaotumia sigara, jambo kuwa ni hatari kwa afya za watumiaji.

Mei 31 ya kila mwaka, ni siku ya maadhimisho ya siku ya kutotumia tumbaku duniani kote lakini bado inaonekana matatizo ya matumizi ya tumbaku na uvutaji sigara yanaongezeka kwa kasi kubwa katika jamii, huku madhara yake yakiwa makubwa ikiwemo maradhi ya kifua kikuu.

Licha ya ukweli kwamba, uvutaji wa sigara ni aina mojawapo ya uvurugaji wa ustaarabu kwa wasiotumia bidhaa hizo, sheria ya nchi inapiga marufuku uvutaji wa sigara hadharani huku suala la kiafya likipewa kipaumbele.

Fikra Pevu imekuwa ikiandika mara kwa mara kuhusu matumizi na madhara ya uvutaji wa sigara kiafya, japo kampuni zinazohusika na shughuli za uzalishaji na utengenezaji zinaiingizia nchi mapato makubwa.

Mnamo mwaka 2003, Bunge la Tanzania lilipitisha sheria inayokataza matumizi ya sigara hadharani, huku ikilenga kukomesha madhara ya kiafya kwa wavutaji wenyewe na wale wanaoathirika kupitia kuvuta moshi wa sigara kutoka kwa wavutaji.

Haya yameelezwa na kufafanuliwa vyema katika Sheria ya Usimamizi wa Bidhaa za Tumbaku, Sura ya 121 TL, ya mwaka 2003, Kipengele cha 12(1).

‘Uvutaji wa sigara ni hatari kwa afya yako’, tahadhari ambayo imebandikwa kwenye pakti za sigara, umekuwa kama wimbo uliozoeleka masikioni mwa watu kuhusu kujulishwa madhara ya sigara, lakini wanapuuzia huku wakihoji kuhusu uwepo wa madhara na wakati huo huo viwanda vinapatiwa vibali vya kufanya biashara hizo za uzalishaji na wakulima wanaendelea kuhimizwa kuongeza uzalishaji.

Kutokana na sheria hiyo kuwepo, japokuwa imekuwa kimya sana ikiwapa mwanya watu kuwa huru kuvuta sigara kwa jinsi wanavyohitaji, imemlazimu Paul Makonda, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, kutoa tamko juu ya jambo hilo.

Tamko hilo la kupiga marufuku uvutaji wa sigara hadharani, linakuja sambamba na zuio la utumiaji wa shisha pamoja na vitendo vya ushoga vilivyoonekana kushika kasi nchini, huku vikipewa kipaumbele cha kuongelewa hata katika vyombo vya habari.

Makonda amewataka wakuu wapya wa wilaya katika mkoa wake kulifanyia kazi jambo hilo na kuwakamata wale wote ambao watabainika wakivuta sigara, shisha na wanaoushabikia ushoga na kuunga mkono kwa kutoa misaada kupitia NGOs.

Katika matoleo yaliyopita Fikra Pevu ilieleza baadhi ya madhara ya matumizi ya sigara na tumbaku, ilipoitaja nchi ya China kuwa na idadi kubwa ya watu Zaidi ya milioni moja wanaokufa kutokana na magonjwa yanayotokana na uvutaji wa sigara na matumizi mengine ya tumbaku.

Aidha, takwimu za Shirika la Afya Duniani (WHO) za mwaka 2003, zinaonyesha kuwa kila baada ya sekunde 10, mtu mmoja hufariki dunia kutokana na maradhi yatokanayo na matumizi ya tumbaku.

Takwimu kutoka (WHO) 2003, zilionyesha kuwa, inakadiriwa kuwa kufikia mwaka 2025, vifo vitakavyotokana na matumizi ya tumbaku vitaongezeka kwa kiwango cha asilimia 70 kuliko ilivyokuwa mwaka 2003.

Pia takwimu hizo zinaonyesha kuwa kufikia mwaka 2030, idadi ya watu milioni 10 watakuwa wakifariki dunia kila mwaka kutokana na uvutaji wa sigara ulimwenguni, huku ikitajwa kuwa asilimia 70 ya vifo hivyo vikitoka katika nchi zinazoendelea, Tanzania ikiwemo.

Wataalamu wa afya wanayataja magonjwa mbalimbali yanayoweza kusababishwa na matumizi ya tumbaku au sigara kuwa ni; saratani ya ngozi, saratani ya mapafu, saratani ya kizazi, saratani ya koo, saratani ya kinywa, saratani ya kibofu, matatizo katika mfumo wa upumuaji, udhaifu katika mifupa (Osteoporosis), kuwahi kumaliza kufikia mzunguko wa hedhi kwa wanawake kabla ya muda wa ukomo, athari kwa wajawazito (kuzaa mtoto njiti), kupungukiwa na vitamin mwilini pamoja na kupungua kwa nguvu za kiume au kike.

Tafiti mbalimbali zinaonyesha kwamba, madhara ya hewa ya tumbaku na sigara si kwa wanadamu pekee, bali hata wanyama na mimea vinaathirika kutokana na moshi huo kwani usambaa kwa haraka kufika mbali kitu ambacho huwezi kugundua kwa njia ya kawaida isipokuwa vipimo maalum vya hewa.

Mwaka 1993, Shirika la Kulinda Mazingira la Marekani (EPA) lilitoa taarifa kukadiria kwamba zaidi ya wanyama 3,000 ikiwemo mimea hupoteza maisha kila mwaka, kutokana na kupokea hewa ya sigara au tumbaku.

Kuvuta moshi unaotokana na mtu mwingine au vitu vingine ambao siyo moja kwa moja, ni hali mojawapo ya uvutaji wa sigara, ambayo madhara yake ni sawa na yule mtu anayevuta moja kwa moja, pia husababisha magonjwa, hivyo basi tamko la mkuu wa mkoa kuzuia uvutaji hadharani utasaidia kupunguza madhara ya kiafya, inabidi liwe mfano kwa mikoa mingine kote nchini ikiwa ni utekelezaji na kuimarisha afya za Watanzania.’

Tuesday 12 April 2016

APOTEZA KICHANGA WODINI


Na Gordon Kalulunga, Mbeya

MTOTO mchanga wa siku nne amefariki dunia katika Hospitali teule ya wilaya ya Mbeya, Ifisi Mbalizi kwa kile mzazi wake alichodai kuwa ni kutopata msaada kutoka kwa wauguzi wa Hospitali hiyo.

Tukio hilo limetokea usiku wa saa sita Machi 27, mwaka huu ndani ya wodi ya wazazi hospitalini hapo.

Akizungumza na Gazeti hili nyumbani kwao baada ya mazishi ya kichanga hicho, mama mzazi wa mtoto huyo Paulina Daud (22), huku akilia alisema kuwa, alipelekwa Hospitalini hapo akiwa mjamzito Machi 24, mwaka huu, majira ya saa tatu asubuhi ambapo saa tano alijifungua kwa njia ya upasuaji.

“Mtoto alikuwa salama na alikuwa akinyonya vizuri nami nikiwa naendelea kuuguza kidonda mpaka tarehe 26 usiku wa saa nne mtoto akawa analia sana ndipo nikaomba msaada kwa muuguzi mmoja akasema yeye hausiki na wodi letu” alisema Paulina.

Alisema pamoja na maumivu ya kidonda chenye mshono, alipoona mtoto anazidi kulia akaamua kujikongoja mpaka chumba cha wauguzi na kuwaeleza tatizo lake, badala ya kwenda kumsaidia wakamwambia aende akamchukue mwanae na kumpeleka chumba walichokuwa wauguzi.

“Nikarudi wodini na kumbeba mtoto kwa shida kisha kumpeleka chumba cha wauguzi na mmoja wa wauguzi akasema nimwamshe mwenzake aliyekuwa amelala pembeni na nilipomwamsha wakamwangalia mwanangu wakasema tayari amefariki” alisema Paulina huku akiangua kilio…

Mama mzazi wa Paulina Sekela Daud, alisema kichanga tangu kipate uhai wake hakikuwa na matatizo yeyote na kwamba, alipopata taarifa ya kifo hicho alishtuka na kuamua kutafuta usafiri kutoka Mbalizi usiku huo na kwenda Hospitalini.

“Nilifika saa kumi na moja alfajiri Hospitalini na niliwaomba walinzi waniruhusu kwa kuwaambia kuwa nilikuwa nimeitwa na wauguzi kwa tatizo la mwanangu, wakaniruhusu na nilipofika nikakuta hali hiyo na nilipowauliza wakasema hawajui sababu yeyote iliyosababisha kifo cha mjukuu wangu” alisema Sekela.

Alisema baada ya taratibu na mabishano kadhaa hospitalini hapo, wakaruhusiwa kutoka na maiti majira ya saa tatu asubuhi na mama mzazi wa kichanga aliruhusiwa kutoka majira ya saa sita mchana na anatakuwa kwenda Hospitalini hapo kutoa nyuzi April 5, mwaka huu.

Machi 29, mwaka huu, mwandishi wa habari hii alifika katika Hospitali hiyo ya Ifisi Mbalizi na kufanya mahojiano na Mganga mkuu mfawidhi wa hospitali hiyo Dr. Msafiri Kimaro, ambaye alisema kuwa hakuwa na taarifa.

Baada ya mahojiano zaidi Dr. Kimaro alimchukua mwandishi na kuongozana naye kwenda wodini kwa ajili ya kuangalia nyaraka ambapo alijiridhisha kuwa mjamzito huyo alijifungua salama na mtoto alikuwa salama lakini pia katika jarada la Paulina wataalam hao wameandika kuwa hawajaona sababu yeyote iliyosababisha kifo cha mtoto huyo.

“Ninakuomba siku ya Alhamisi (Machi 31, mwaka huu), ufike kwa ajili ya taarifa zaidi ili nifuatilie” alisema Dr. Kimaro.

Machi 31, mwaka huu, tayari timu ya wataalam kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mbeya ilifika katika hospitali hiyo kuhoji jambo hilo na mengine ambayo gazeti hili linaendelea kujiridhisha likiwemo mwanamke aliyefanyiwa upasuaji na kushindwa kushonwa vizuri na sasa tumbo lake limeanza kuvimba na anatakiwa kufanyiwa upasuaji mpya ili ashone vyema katika hospitali ya wazazi Meta.

April mosi mwaka huu, mwandishi alifika tena hospitalini hapo na kukutana na Mganga Mkuu wa Hospitali hiyo Dr. Msafiri Kimaro na Katibu wa Hospitali hiyo, Dick Balagasi, ambapo walisema maelezo yote mwandishi anapaswa kuyapata kwa wauguzi waliokuwa zamu maana wao hawakuwepo siku tukio hilo likifanyika.

“Kalulunga lakini unapaswa kudumisha mahusiano na nasi maana tumeambiwa kuwa unaishi jirani hapa, hivyo ni vema tukadumisha mahusiano kuliko ukisikia jambo unaandika” alisema Balagasi kabla hajakatishwa na kauli ya mwandishi wa habari kuwa “Hisia zisiondoe uhalisia”.

Hata hivyo ikumbukwe kuwa, mtindo wa uongozi wa Hospitali hiyo kuwa na kifua kikubwa cha kuwatetea baadhi ya watumishi wanaoshindwa kuwajibika vizuri ulisababisha mjamzito Sabina Mwakyusa (28), kufukuzwa wodini na kujifungulia katika geti la hospitali hiyo kwa msaada wa walinzi huku mvua ikinyesha usiku.

Tukio hilo lilitokea usiku wa Desemba 19, mwaka 2013, ambapo baadhi ya wauguzi waliokuwepo katika chumba cha matazamio ya kujifungua, walidaiwa kumfukuza na kumpiga mjamzito Sabina Mwakyusa(28) mkazi wa Kijiji cha Iwala, kata ya Utengule Usongwe wilayani humo.

Sabina, alisema alifika hospitalini hapo Desemba 18, 2013 na alipimwa na manesi ambapo walimwambia kuwa hawamuoni mtoto tumboni mwake.
‘’Baadaye akaja Daktari na kunipima, akaniambia mtoto anaonekana vizuri na ningejifungua mtoto wa kike ndipo nikaendelea kusubiri uchungu zaidi’’ alisema Sabina.

Alisema ulipofika usiku wa Desemba 19 majira ya saa mbili usiku, alianza kujisikia uchungu, ndipo manesi waliompima mwanzo wakamwambia anatakiwa apimwe tena jambo ambalo alikataa kwa madai kuwa alikuwa akiumizwa, ndipo wakamwambia aondoke hospitalini hapo kwasababu ana kiburi.

‘’Baada ya kuonekana mimi nasita kuondoka, wakaanza kunipiga na kunipatia biki na kunilazimisha kuandika kuwa mimi sitaki kujifungulia hapo ndipo tukatoka na mama na kwenda nje ya geti na kujifungulia getini huku mvua ikinyesha’’alisema Sabina Mwakyusa.

Alisema, mama yake na baadhi ya wajawazito waliokuwepo ndani ya wodi hilo, walijaribu kuwabembeleza wasimfukuze lakini walikataa. 

Mama mzazi wa mwanamke huyo, Roda Mwakyusa(50), alisema anaumia akikumbuka yaliyomkuta mwanaye ikiwa ni uzao wake wa kwanza.

‘’Niligaragara mweeeh! kuwaomba msamaha wale manesi ili wamsamehe na kumhurumia huyu mtoto wangu, lakini walikataa wakisema kuwa ana kiburi sana’’ alisema Prisca Mwakyusa.

Alisema walipotoka wodini huku mwanaye uchungu ukimzidi, walifika getini akazidiwa. Chupa ikapasuka. Damu zikaanza kumvuja; alikaa muda mrefu zaidi ya saa moja na kuanza kujifungua ndipo walinzi wa kampuni ya Mult-Lion, wakamsaidia kumpeleka katika upenu wa duka la hospitali hiyo ili kukwepa kokoto zilizopo na mvua iliyokuwa ikinyesha.

Mkurugenzi wa kampuni ya ulinzi ya Mult-Lion, Kinanda Sanga, alipoulizwa kuhusu tukio hilo, alisema kuwa hakuwa na taarifa lakini baada ya kuwauliza askari wake walimpatia taarifa ya tukio hilo kuwa lilitokea na wao wakatoa msaada.

Dada wa msichana huyo, Enitha Mwakyusa(35), alisema alipigiwa simu majira ya saa tano usiku na mama yake mzazi akimweleza yaliyomkuta mdogo wake na kwamba atafute gari la kwenda kuwachukua.

‘’Mama alinipigia simu usiku, nikawaamusha majirani ambao walikuwa na namba za madereva tax, ambapo saa saba walifika hapa nyumbani Mapelele’’ alisema Enitha.

Wifi wa Sabina Mwakyusa, Prisca Nafred, alisema alimpeleka mtoto aliyezaliwa katika hospitali hiyo majira ya saa saba mchana ya Desemba 20, kwa ajili ya chanjo, lakini hakupata chanjo kwa madai kuwa alikuwa amechelewa kufika, hivyo alitakiwa kufika siku ya Jumanne Desemba 24, mwaka huo.

Desemba 21, familia hiyo ilimpigia simu Mwandishi wa habari wakimweleza kuhusu maendeleo mabaya ya mtoto ambapo Mwandishi wa habari hizi alimtaarifu Mratibu wa afya ya mama na mtoto mkoa wa Mbeya, Prisca Butuyuyu, kuhusu suala hilo ambapo makubaliano yaliafikiwa kuwa mtoto apelekwe Hospitali ya Rufaa, kitengo cha wazazi Meta.

Mtoto huyo alipokelewa Meta na kuingizwa kwenye chumba cha joto kisha kuanza kupatiwa matibabu kwa kuwekewa drip za maji mpaka Desemba 23 mwaka huu.

Mganga Mkuu wa wilaya ya Mbeya Louis Chomboko, alipopata taarifa, alichukua hatua ya kwenda kumuona mtoto huyo katika hospitali ya Meta.
‘’Nimeonana na mama wa mtoto na kumuona mtoto chumba cha joto na kupata maelezo yote ikiwa ni pamoja na maelezo ya file la Meta hivyo nipe nafasi tena kufuatilia tukio hili hospitali ya Ifisi na tukibaini ukweli tutachukua hatua’’ alisema Dr, Chomboko akimsihi Mwandishi kutoandika kwanza habari hii.

Mwezi Desemba mwaka 2012, Mama mmoja(jina tunalo), aliyekuwa anaumwa BP, alichomwa sindano (dawa)ambazo haziendani na ugonjwa wake na mmoja wa watoto wake alipohoji kwa uongozi wa hospitali hiyo alijibiwa kuwa hapaswi kugombana na wauguzi! Kisha akaitwa Dr. Kenneth, ambaye aliamua kuokoa maisha ya mama huyo katika hospitali hiyo ya Ifisi kwa kumchoma sindano ya dawa iliyokuwa ikitakiwa.

Announcement: Applications for content and rural dispatch grants now open


April 06, 2016  |   accountability,capacity building,Frontpage,media,rural,tanzania   |     |   Comments Off on Announcement: Applications for content and rural dispatch grants now open
Tanzania Media Foundation is pleased to announce that it will now be receiving applications for the Rural Dispatch and Content grant.

The Rural Dispatch grant, whose recipients may come from rural or urban areas, aims to increase to increase quality, quantity and diversity of rural voices and issues of ordinary people in the media. It was successfully offered to more than 500 journalists under the Tanzania Media Fund project, whose work is now being conducted by the new TMF.

This year, TMF will issue 60 of the total 150 grants it expects to issue to journalists during the implementation of its 2015 – 2018 strategic plan. This call is specifically directed at journalists who opt not to go through the ideation process which TMF will conduct with journalists later in April. Ideation is a process through which journalists pitch their story idea to a mentor who then helps them to strengthen and improve it. Thereafter, the mentor makes a recommendation to TMF on the quality of the story idea.

 Following TMF’s February and March outreach to journalists in 19 regions across Tanzania, the organisation expects from April 18, 2016 to provide ideation to over 500 journalists, based on registration.

The Content Grant is also a continuation of the institutional grants issued under the Tanzania Media Fund project. The objective of this grant is to enable both non-media outlets – such as independent producers, media associations/organizations and training institutes – and media outlets to produce specialised, well-researched quality content. TMF aims to 30 content grants, each valued at USD100,000, during the current strategic period (2015-2018). This year, the organisation will issue nine grants of this kind.
 
Deadline for applications is 5th May, 2016. All applications for these grant categories must be made online, through TMF’s Flexi-grant system, available on https://tmf.flexigrant.com.
For more information, access the calls on the links below:
  1. Call for rural dispatch grant applications
  2. Call for content grant proposals
To avoid disqualification, carefully read and follow the instructions on how to apply.