Watoto kama hawa wanastahili kuendelezwa vipaji vyao kama wanavyoonekana, hawana viatu lakini duh! mambo safi.
Tusiuze wala kujenga katika maeneo ya wazi ambayo watoto wanacheza.
Saturday 14 November 2015
Dawa za kulevya zaleta uchugu kwa vichanga na wajawazito Tanzania
DAWA za kulevya ni kemikali za majimaji, majani au unga wenye kemikali zenye vilevya, ambazo zikitumiwa na viumbe, hubadili hisia, fikra na tabia ya mtumiaji, akiwemo binadamu na viumbe vingine.
Zinaweza
zikawa halali au si halali, asili au zinazotengenezwa kiwandani, katika mfumo
wa vidonge, unga au maji, zikatumika kwa njia ya kujidunga, kunusa, kula, kunywa,
kuvuta, au kupiga bamba.
Dawa hizo
zimegawanyika katika makundi makuu matatu ambayo yanatenganishwa kutokana na
jinsi dawa hizo zinavyoathiri mfumo wa utendaji kisaikolojia (psychoactive
substance).
Makundi hayo
ni Vichangamshi (Stimulants) mfano; cocaine, tumbaku na khat.
Kundi la pili ni Vipumbaza (Depressants), mfano; pombe, heroine, methadone, codeine, morphine, na gundi.
Kundi la
tatu ni Vileta Njozi (Hallucinogens). Mfano ; uyoga, bangi.
Wanawake wajidunga
waeleza yaliyowapata wakati wa ujauzito.
Baadhi ya
wanawake wanaotumia dawa za kulevya Jijini Dar es Salaam, na walioacha kutumia,
wanaeleza adha na changamoto wanazozipata katika maisha yao ndani ya jamii.
Wanasema,
walijitumbukiza katika matumizi ya dawa hizo bila kujua kuwa ni utumwa na
ugonjwa mbaya.
Fatuma
Athuman, mama wa mtoto mmoja wa kike, anasema alianza kutumia dawa za kulevya
aina ya Heroin kwa kuchanganya na sigara huku akivuta, kisha akaanza kujidunga
na sindano na hatimaye Baba yake akamfukuza nyumbani, akaenda mitaani ambako
pia alikuwa akiambulia mateso ya polisi ya kukamatwa na kupigwa.
“Mwaka 2012
ndipo nilipotamani kuacha kutumia dawa za kulevya, nikajipeleka kwenye tiba ya
Methadone inayopatikana Mwananyamala, Temeke na Muhimbili, Jijini Dar es
Salaam, kwa sasa naendelea vizuri”anasema Fatuma Athuman.
Fatuma
Side(31), anasema alianza kutumia bangi akiwa na miaka 25, na hakuwa na mtoto,
baadaye akaaza kutumia Cocain na sasa ana mtoto.
“Nilipata
mimba nikiwa nyumbani, lakini kipindi hicho nilikuwa nashinda sana maskani
kuvuta. Nilipojifungua nikaendelea kwenda na mtoto huko maskani, lakini
ikanishangaza mtoto alipoanza kupata akili, akawa anaiga vitendo vyote
tulivyokuwa tukifanya maskani…, nikaanza kumwacha nyumbani kwa wazazi wangu ili
asiharibike”anasema Fatuma Side.
Anasema
katika maisha yake ya utumizi wa dawa za kulevya, anakumbuka kuwa aliuza vitu
vyake vya ndani ili ajipatie pesa kwa ajili ya
kununua dawa za kulevya!
Wajawazito na ulalaji
katika maskani za kuvutia dawa za kulevya
Fatuma
anasema, ulalaji wa wanawake wenye mimba na watoto huko maskani siyo mzuri, mwanamke mmoja analala
katikati ya wanaume kumi, huku mtoto akiwa anapigwa na baridi kwa sababu siku
nyingine usiku kunakuwa na baridi kali, huku wengine wakiendelea kuvuta bangi
na wengine wakijidunga.
“Ukiwa na
mtoto mdogo maskani ni shida sana, unalala mwanamke peke yako katikati ya
wanaume kumi huku mtoto mchanga akipigwa na baridi, unaamka asubuhi mama mtu
miguu ikiwa imevimba na wakati huo huo utakuta umelala saa nane usiku baada ya
kutoka labda stereo au Muhimbili kutafuta unga” anasema Fatuma Side.
Anaeleza
kuwa amewahi kukamatwa na askari polisi na kupelekwa gereza la segerea kwa siku
ishirini, ambako anasema maisha ya huko hayana utu kabisa, kisha siku ya
ishirini alipopelekwa mahakamani akaachiwa huru.
Anasema,
mtumiaji wa dawa za kulevya ana hatari ya kupata maambukizi ya VVU na homa ya
ini B na C, kutokana na ngono na udungaji usio salama ambao unasababishwa na
matumizi ya kuchangia sindano za kujidungia na kwamba uzoefu wake mpaka sasa
wengi wa wajidunga wana maambukizi ya VVU na kifua kikuu kutokana na tabia za
kulundikana kulala na kufanya ngono zisizo salama na baadhi ya wanawake kufanya
biashara ya ngono isiyo salama.
Kwa sasa
anasema ameacha kutumia dawa za kulevya, kutokana na msaada na huduma
anazozipata kutoka shirika la Medecins du Monde (MDM), na anaishi kwenye nyumba
yake aliyojenga, bado hajaolewa, wadogo zake na wazazi wakimuona hawalii tena,
jamii inamuheshimu si kama zamani.
Kwa sasa
nimwelimishaji rika wa MdM na ana wahudumia wenzake kwa kuwapa elimu ya afya,
kondomu na vifaa salama vya kujidungia hasa ambao wanaendelea kutumia dawa za
kulevya na anasema wengi wanabadilika ikiwemo kupunguza matumizi na kuacha
kabisa kama yeye.
Mbali na
huyo, Salima Hamad (30), anasema yeye amevuta bangi kwa kuchanganya na heroin
kwa miaka 14, na amejidunga kwa muda wa miaka 5.
Anasema
“nilipo anza kutumia dawa za kulevya, mwanzoni hakuna aliyegundua, siku
zilivyokwenda nilianza kudhoofika kiafya, mama aliambiwa kuwa mwanao anatumia
dawa za kulevya, aliponiuliza, nikamkatalia lakini siku zilivyokwenda afya
yangu ilianza kudhoofika, nyumbani walithibitisha kuwa natumia dawa za kulevya
walikuwa wakinisema sana, nikaondoka nyumbani,”anasema Salima.
Anasema
katika maisha ya utumiaji wake, alinyanyapaliwa, kila alipokuwa akipita hasa
maeneo ambayo wanamfahamu alikuwa anasemwa vibaya kwa dharau kuwa siku hizi ni
mwizi, mtu yeyote asimuamini.
“Niliumia sana,
kwani hakuna mtu aliyekuwa akiniamini, kwani jamii ishakuwa na mtazamo kuwa
kila mtumiaji wa dawa za kulevya ni mwizi”.anasema.
Yeye akiwa
mwanamke mtumiaji wa dawa za kulevya, alipokuwa mjamzito kwa mara ya kwanza
hakuwahi kwenda kliniki kwa sababu ya hofu ya kuwaeleza wahudumu jinsi gani
wangeweza kumwelewa wakati hakuwa na fedha.
“Kwa
muonekano wangu, nilijipa majibu kuwa nesi hawezi kunijali, kwahiyo niliendelea
na maisha ya maskani mpaka nikajifungulia huko huko, sikuwa na chakula cha
mtoto, hivyo hivyo nikipata haya, nikikosa sawa, huku nilikuwa nikiendelea
kutumia dawa za kulevya” anasema Salima.
Alipoulizwa
kuwa nani alimsaidia wakati wa kujifungua, anasema ni wenzake.
Dr. Moke Magoma wa shirika la Evidence For Action(E4A) linaloshughulika na mradi wa kuokoa maisha ya mama na mtoto nchini(Mama Ye!), ambaye ni mbobevu wa masuala ya afya ya uzazi, anasema robo tatu ya wajawazito wanaobeba mimba na kujifungua, wanajifungua salama bila hata wasaidizi wenye ujuzi bali robo inayobaki ndiyo wanapata shida na baadhi kufariki.
Dr. Moke Magoma wa shirika la Evidence For Action(E4A) linaloshughulika na mradi wa kuokoa maisha ya mama na mtoto nchini(Mama Ye!), ambaye ni mbobevu wa masuala ya afya ya uzazi, anasema robo tatu ya wajawazito wanaobeba mimba na kujifungua, wanajifungua salama bila hata wasaidizi wenye ujuzi bali robo inayobaki ndiyo wanapata shida na baadhi kufariki.
“Bahati
mbaya ni vigumu kuwatambua wale robo kwasababu matatizo hutokea ghafla na bila
kutegemewa hivyo haja ya akina mama wajawazito kuhudhuria kliniki na
kujifungulia katika vituo vya afya vyenye wataalam wenye ujuzi wa ukunga ni
muhimu ingawa bahati mbaya bado kuna vituo hasa vijijini havina wataalam maana
siyo kila mhudumu ni mkunga” anasema Dr. Moke Magoma.
Katika ujauzito wake wa pili, Salima anaeleza kuwa akafahamu kuwa kuna shirika la MdM linalosaidia wajidunga, alikwenda huko na akahudumiwa kama mtoto, akapelekwa hospital, akapatiwa vifaa vya kujifungulia na akawa anafuatiliwa mpaka akajifungua huku akipatiwa pia unga wa uji na chakula cha kwake na mtoto.
Kwa sasa
anasema anatumia dawa aina ya methadone, inayosaidia kupunguza kiasi cha
matumizi ya dawa za kulevya na kuacha, anasema amebadilika hata mwili wake,
anaenda kwenye kituo cha MdM kupatiwa elimu na kupimwa kuangalia hali yake ya
maambukizi.
“Kwa ufupi kutokana na mradi huu tunaonekana sasa watu, hata nikienda nyumbani wanaongea na mimi kama mtu mwingine”anasema.
Mtaalam wa
mifumo ya kompyuta katika Tume ya uratibu na udhibiti dawa za kulevya Tanzania
bara, January Ntisi, (DCC), anasema matumizi ya dawa za kulevya nchini
yanasababishwa na sababu tofauti ikiwemo makundi rika, unyanyasaji wa
kisaikolojia wanaofanyiwa watu, upungufu wa maadili mema, ushawishi, kuonesha
ufahari na mambo mengi.
Anasema,
urefu wa ukanda wa bahari wenye vipenyo vingi ni moja ya sababu ya dawa hizo
kuendelea kuingia nchini.
Uchunguzi wa
gazeti hili, umebaini kuwa, mazingira ya bandari ya Zanzibar ni tatizo katika
kufanikisha kupunguza uingizaji na utumiaji wa madawa ya kulevya kutokana na
bandari hiyo kuwa wazi kiasi ambacho mtu yeyote anaweza kuingiza kitu chochote
nchini mbali na dawa za kulevya.
Ofisi ya
kamanda wa polisi Mkoa wa Unguja Zanzibar, inakiri kuwa, uingizaji wa boti
zaidi ya moja kwa wakati mmoja bandarini ni moja ya kikwazo katika kupambana na
wahalifu na kwamba mazingira ya Kijiografia ya visiwa vya Zanzibar yanachangia
kwasababu kuna zaidi ya bandari 500 za kienyeji Unguja pekee, ambazo zinaweza
kuingiza madawa ya kulevya kwa kutumia vyombo vidogo vidogo vya kienyeji wakati
wowote ule wapendao, na kwa sababu Polisi haina vyombo vyovyote vya kufanyia
doria ni vigumu kufika maeneo kama hayo ambayo kwa hakika yanatakiwa uangalizi
wa mara kwa mara.
Watumishi wa MDM
waeleza huduma waitoayo
Mfanyakazi
(Outreach Worker) wa shirika la Medecins du Monde(MdM) la wilayani Temeke, Aina
Mrope, anasema anaumia kuwaona wanawake wanaotumia dawa za kulevya huku wakiwa
na familia.
“Tunawaendea
hata majumbani na kuwasaidia kuwapa elimu ya afya ya uzazi ikiwa ni pamoja na
kuwapeleka hospitali wale wanaoumwa na kuwapatia kondomu wale ambao wanafanya biashara
ya ngono”anasema Aina.
Anasema
wanawake wanaotumia dawa hizo za kulevya na kuhudumiwa na kituo chao,
wanapatiwa pia pamba, nguo, chakula, dawa za nywele, mafuta, vipodozi na kila
siku kuu wanapatiwa mavazi.
Mshauri wa
masuala ya saikolojia wa shirika hilo la MDM, Benjamin Myovela, anasema moja ya
kazi zinazofanywa na kitengo chake ni kuwashauri watumiaji madhara ya udungaji
usio salama na hatari zake, ambapo jambo la kuamua kuacha au kuendelea ni la
muhusika mwenyewe, lakini akiwa bado anatumia atumie kwa njia ya usalama ili
asipate maambukizi ya VVU na homa ya ini B na C au matatizo mengine ya kiafya.
Mshauri wa
masuala ya afya wa shirika hilo, Prof. Joseph Mbatia, anasema kuwa kundi la
wanaotumia dawa za kulevya lipo katika hatari kubwa ya maambukizi ya VVU.
Anasema
kundi hilo likiachwa bila kupewa elimu na kusaidiwa katika matibabu na
kujikinga, jamii itakuwa kwenye hatari zaidi kwasababu kuna baadhi wanafanya
biashara ya ngono.
“Kuna
wanawake wanaotumia dawa za kulevya na kufanya biashara ya ngono kwa lengo la
kupata fedha, wanakutana na watu ambao hawatumii ambao pia endapo mwanamke huyo
ana maambukizi, jamii nzima inakuwa hatarini” anasema Prof. Mbatia.
Meneja wa
mafunzo wa shirika hilo, Damali Lucas, anasema“matatizo kwa wanawake
wanaoutumia dawa za kulevya ni mengi sana, muda mwingi jamii inawalaumu na
kuona kuwa maisha wanayoishi wanajitakia au wamependa.
“Kama jamii hatukumbuki kuwa kuna wengine wameingia katika matumizi ya dawa za kulevya kwa ushawishi kutoka kwa wapenzi wao, wamefiwa wazazi wao, kwa hiyo hawakuwa na uangalizi mzuri.” Anasema Damali.
Anasema,
wanawake wanaotumia dawa za kulevya wanakumbwa na matatizo ya unyanyasaji wa
kijinsia kwa kupigwa hasa na wapenzi au hata watu kutoka kwenye jamii,
wanachukuliwa kama wamama ambao hawawezi kulea watoto, kuna wengine
wakijifungua watoto wananyang’anywa kwa madai hawawezi kulea.
“Kwa sasa
MdM inajitahidi sana kuwafikia wanawake wanaotumia dawa za kulevya popote
walipo majumbani kwao na kituoni kwa sababu kutokana na utafiti uliofanyika
kiwango cha maambukizi ya VVU kwa wanawake wanaotumia dawa za kulevya kipo
zaidi ya asilimia 60%, kwa hiyo ni hatari sana kwa afya ya jamii kwasababu
wanaingiliana na watu wa kawaida hata kwenye masuala ya kingono” anasema
Damali.
Pia anasema
MdM inatoa huduma za kisheria kwa wanawake wajidunga na walioacha kutumia dawa
za kuelvya, huduma za afya ya uzazi, tiba na ushauri wa kisaikolojia ili wawe
na afya bora na kuheshimika kama wanawake wengine.
Taarifa ya
hali ya dawa za kulevya nchini ya mwaka 2011, iliyotolewa na tume ya kuratibu
udhibiti wa dawa za kulevya, chini ya ofisi ya Waziri Mkuu, kwa mujibu wa
kifungu cha 6 cha Sheria ya kuzuia biashara haramu ya dawa za Kulevya [Sura ya
95], inaonesha kuwa, dawa za kulevya zinazotumiwa kwa wingi nchini ni bangi
ikifuatiwa na mirungi, heroin na cocaine.
Dawa
nyingine ni kama vile gundi na petrolpamoja na dawa za tiba zenye madhara ya
kulevya zikiwemo valium, morphine na napethidine.
Inasema
kuwa, matumizi ya dawa hizi yamejikita zaidi katika mikoa ya Dar es Salaam,
Tanga, Arusha, Mwanza, Mbeya, Iringa na Morogoro ambapo wengi wa watumiaji ni
vijana wa kiume wenye umri kati ya miaka 12-35.
Taarifa hiyo
inasema kuwa, matumizi haya hufanyika kwa siri katika maeneo mbalimbali
yakiwemo makaburini, mageto, majengo yasiyokamilika, magofu, vijiweni na
viwanja vya michezo.
Makala hii
imeandikwa kwa msaada wa mfuko wa vyombo vya habari Tanzania(TMF), Tume ya
kuratibu udhibiti wa Dawa za kulevya nchini(DCC) na Dawati la Umoja wa Mataifa
la kupambana na mihadarati na uhalifu (UNODC).
Mwandishi wa
makala 0754 440749
Email;
kalulunga2006@gmail.com
FISTULA YATESA WANAWAKE MBEYA.
Mkurugenzi wa Shirika hilo Gordon Kalulunga (kushoto).
Mbeya Vijijini na Mbozi vinara ugonjwa wa Fistula.
- Serikali itoe elimu na kuwatibu wagonjwa.
- Mwanamke mmoja ang’olewa kizazi.
ASASI isiyokuwa ya Kiserikali ya Tanzania
Community Media Organization (TACOMO) yenye makao makuu mkoani Mbeya,
imesema ugonjwa wa matundu sehemu za siri kwa wanawake (Fistula) umekuwa
mkubwa mkoani humo hivyo Serikali inatakiwa kuvalia njuga ugonjwa huo
unaotibika.
Wakizungumza na waandishi wa habari
mkoani Mbeya, viongozi wa asasi hiyo wamesema asasi yao imefanya
uchunguzi kwa zaidi ya mwaka mmoja sasa na kubaini maeneo yenye wagonjwa
wengi wa Fistula ikiwemo wilaya ya Mbeya Vijijini na Mbozi.
Mkurugenzi mtendaji wa shirika hilo
Gordon Kalulunga alisema katika wilaya hizo baadhi ya maeneo ndiyo
ulikotopea(komaa) ugonjwa huo na wanawake wengi wanashindwa kujitokeza
kutibiwa ugonjwa huo kutokana na elimu duni ya matibabu ya ugonjwa huo
ambao matibabu yake yanatolewa bure na Serikali.
Kalulunga alizitaja wilaya za Mbozi na
Mbeya Vijijini kuwa ni wilaya za mkoa wa Mbeya zenye wagonjwa wanawake
wengi walioathiriwa na ugonjwa huo wa Fistula hivyo Serikali kupitia
Wizara ya Afya inapaswa kuchukua hatua za makusudi kuwarejeshea utu
wanawake wenye matatizo hayo ya Fistula kwa kuanzisha kampeni yenye tija
kwa kushirikiana na Hospitali teule ya Ifisi na Hospitali ya Rufa ya
Mbeya kitenmgo cha wazazi Meta.
Aidha alisema mbali na kushirikiana na
Hospitali hizo pia Serikali iongeze wataalam katika Hospitali hizo wenye
uwezo wa kutibu Fistula tofauti na sasa ambapo Hospitali hizo zina
Mganga mmoja mmoja wenye uwezo wa kutibu ugonjwa huo.
‘’Tumefanya uchunguzi wa muda mrefu tangu
mwezi Mei mwaka 2010 na kubaini kuwa wanawake wengi katika wilaya hizo
wana Fistula lakini hawajajitokeza kutibiwa kwa kuogopa na wanatengwa
katika shughuli za kijamii na baadhi wamekimbiwa na waume zao hivyo
tunaiomba Serikali ichukue Jitihada za makusudi kuanzisha kampeni za
kuwasaidia wanawake hao zitakazopelekea kupata matibabu na ikiwezekana
matangazo yatengenezwe na Haki Elimu’’ alisema Kalulunga.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa asasi hiyo
Angelica Sullusi alisema ugonjwa huo hutokana na jeraha wanalopata kina
mama wakati wa kujifungua baada ya kupata uchungu kwa muda mrefu na pia
kuwa na njia ndogo ya uzazi kiasi kwamba kichwa cha mtoto kinashindwa
kupita kwa usalama wakati wa kujifungua.
Mgandamizo huo wa mtoto husababisha tundu katika njia ya uzazi na kibofu cha mkojo na mara nyingine katika njia ya haja kubwa na kusababisha muathirika kutoka na haja hizo bila ya mpangilio au kujizuia.
Kutoka huko na haja ovyo, huacha unyevunyevu mwingi katika sehemu za siri na kusababisha harufu mbaya. Wengi wenye tatizo hili hulazimika kuishi kwa hali ya aibu na mara nyingine hutengwa na wanaume zao na jamii inayowazunguka.
Sanjari na hilo Sullusi alisema kwa mujibu wa Shirika Afya Duniani (WHO) takriban wanawake milioni nne ulimwenguni kote wanaishi na fistula na wengine 50,000 hadi 100,000 wanapata tatizo hilo kila mwaka na wengi wao wanaishi barani Afrika.
Mgandamizo huo wa mtoto husababisha tundu katika njia ya uzazi na kibofu cha mkojo na mara nyingine katika njia ya haja kubwa na kusababisha muathirika kutoka na haja hizo bila ya mpangilio au kujizuia.
Kutoka huko na haja ovyo, huacha unyevunyevu mwingi katika sehemu za siri na kusababisha harufu mbaya. Wengi wenye tatizo hili hulazimika kuishi kwa hali ya aibu na mara nyingine hutengwa na wanaume zao na jamii inayowazunguka.
Sanjari na hilo Sullusi alisema kwa mujibu wa Shirika Afya Duniani (WHO) takriban wanawake milioni nne ulimwenguni kote wanaishi na fistula na wengine 50,000 hadi 100,000 wanapata tatizo hilo kila mwaka na wengi wao wanaishi barani Afrika.
Pia alisema kuwa tatizo la Miundombinu
mibovu na uhaba wa zahanati hasa vijijini pia ni sababu inayochangia
wanawake kutopata huduma za Afya ya uzazi kwa wanawake ambapo hata
ushirikiano wa wazazi wenza yaani wanaume juu ya kuwasaidia wake zao
wakati wa kujifungua ni mdogo mno.
Sullusi alisema pamoja na hayo asasi hiyo
inaandaa kongamano la kuhamasisha wananachi ili kujenga utamaduni wa
kwenda katika zahanati na Hospitali kupata elimu ya Afya ya uzazi kuliko
hivi sasa ambapo watanzania wengi huanza kupata elimu hiyo wanapopata
ujauzito hasa mjini hivyo ameiomba Serikali navyombo vya Habari kuunga
mkono jitihada za asasi hiyo kwa ajili ya kupunguza uwezekano wa kutokea
Fistula kwa wanawake.
Kushoto ni Mweyekiti wa TACOMO Angelica Sullusi akiwa anajadiliana jambo na Mkurugenzi mtendaji wa Shirika hilo Gordon Kalulunga mwaka 2011.
TACOMO NI SHIRIKA LISILO LA KISERIKALI NCHINI TANZANIA
Shirika letu linaitwa Tanzania Community Media Organization (TACOMO).
TUNAPENDA kutoa shukrani zetu za dhati kwa kutupokea katika njia hii ya mawasiliano kupitia mtandao.
TACOMO PROFILE
JINA KAMILI;
Tanzania
Community Media Organization.
KIFUPI;
Tacomo.
MWANZILISHI NA KIONGOZI MKUU;
Gordon Frank
Kalulunga.
MWAKA WA KUANZA;
2010.
MWAKA WA USAJILI;
Julai 6,
2011.
NAMBA YA USAJILI;
OoNGO/oooo4650
ILIKOSAJILIWA;
Wizara ya
jamii jinsia na watoto.
MAHALA TULIPO;
Mbalizi,
wilaya ya Mbeya (Vijijini) mkoa wa Mbeya.
LENGO NA MADHUMUNI;
Lengo la
shirika ni kusaidia jitihada za serikali katika kuwezesha jamii katika
kuibua na kutatua baadhi ya changamoto za kimaendeleo katika nyanja
mbalimbali zikiwemo za ulinzi wa mtoto, vijana, wazee, jinsia, Afya, Mazingira,
Kilimo na kuandaa warsha/ mafunzo, kushiriki na kushirikishwa katika
shughuli za kimaendeleo na uwezeshaji kwa vikundi
mbalimbali kwa lengo la kutokomeza umasikini.
Aidha
tunashiriki na kushirikishwa katika kuunganisha jamii kwa lengo la kutokomeza
umasikini na kuibua hoja kisha kuifikishia serikali kupitia vyombo vya habari.
KAZI ZA SHIRIKA;
Moja ya kazi
za shirika letu ni kuibua vyanzo vinavyochangia kutokuwa na huduma bora za Afya
ikiwemo matatizo ya wanawake, Ulinzi wa watoto ukatili wa kijinsia na kupatanisha jamii
zilizofarakana.
MAHALI PA KAZI;
Shirika
limesajiliwa kufanya kazi mahala popote Tanzania bara.
MAFANIKIO;
Tangu
shirika letu lisajiliwe kisheria, tumeweza kushiriki na kuhamasisha vijana
kujiunga katika vikundi vya kujitolea na vya ujasiliamali ambapo mafanikio
makubwa yanaonekana katika kikundi cha usafi na uhifadhi wa mazingira mkoa wa
Mbeya kiitwacho Umoja wa Vijana Wazalendo Mbeya (UVIWAMBE), ambacho awali
walikuwa wanajitolea lakini kwa sasa wananufaika baada ya kupewa kibali cha
kukusanya tozo za usafi katika mji mdogo wa Mbalizi, Halmashauri ya wilaya ya
Mbeya.
Aidha tunashirikina
vema na Halmashauri ya wilaya ya Mbeya katika kujumuika katika ushawishi wa
wananchi kuunda vikundi na ushawishi wa kuchangia maendeleo.
Tumeweza
kuwachukua na kuwalipia mafunzo ya uchoraji (Artist) watoto na waliokuwa wa
mitaani zaidi ya 10 ambao ni chini ya miaka 17 ambao kwa sasa baadhi wanajitegemea
na mmoja bado yupo mafunzoni kwa vitendo kupitia mchoraji Asia Print wa Mbeya kwa
michango yetu wenyewe kama wanachama.
Kwa sasa
tuna vijana wanne wa mitaani ambao tunawalipia mafunzo ya kuendesha pikipiki
(Boda Boda) na kila baada ya miezi mitatu tunatembelea hospitali kuona
wagonjwa.
MAWASILIANO YA SHIRIKA
Tanzania
Community Media Organization (TACOMO).
S.L.P 705,
Mbeya-Tanzania,
SIMU; 0754
440749/0655 440749/0765 615858
EMAIL; tacomotz@gmail.com
Tunaahidi kuwapa ushirikiano mkubwa katika kujuzana taarifa mbalimbali za kimaendeleo.
Subscribe to:
Posts (Atom)