Saturday 14 November 2015

TACOMO NI SHIRIKA LISILO LA KISERIKALI NCHINI TANZANIA


Shirika letu linaitwa Tanzania Community Media Organization (TACOMO).

TUNAPENDA kutoa shukrani zetu za dhati kwa kutupokea katika njia hii ya mawasiliano kupitia mtandao.



TACOMO PROFILE
JINA KAMILI;
Tanzania Community Media Organization.

KIFUPI;
Tacomo.

MWANZILISHI NA KIONGOZI MKUU;
Gordon Frank Kalulunga.

MWAKA WA KUANZA;
2010.

MWAKA WA USAJILI;
Julai 6, 2011.

NAMBA YA USAJILI;
OoNGO/oooo4650

ILIKOSAJILIWA;
Wizara ya jamii jinsia na watoto.

MAHALA TULIPO;
Mbalizi, wilaya ya Mbeya (Vijijini) mkoa wa Mbeya.

LENGO NA MADHUMUNI;
Lengo la shirika ni kusaidia jitihada za serikali katika kuwezesha jamii  katika kuibua na kutatua baadhi ya changamoto za kimaendeleo katika nyanja mbalimbali zikiwemo za ulinzi wa mtoto, vijana, wazee, jinsia, Afya, Mazingira, Kilimo na kuandaa warsha/ mafunzo, kushiriki na kushirikishwa katika shughuli za kimaendeleo na uwezeshaji kwa vikundi mbalimbali kwa lengo la kutokomeza umasikini.



Aidha tunashiriki na kushirikishwa katika kuunganisha jamii kwa lengo la kutokomeza umasikini na kuibua hoja kisha kuifikishia serikali kupitia vyombo vya habari.

KAZI ZA SHIRIKA;
Moja ya kazi za shirika letu ni kuibua vyanzo vinavyochangia kutokuwa na huduma bora za Afya ikiwemo matatizo ya wanawake, Ulinzi wa watoto ukatili wa kijinsia na kupatanisha jamii zilizofarakana.

MAHALI PA KAZI;
Shirika limesajiliwa kufanya kazi mahala popote Tanzania bara.

MAFANIKIO;
Tangu shirika letu lisajiliwe kisheria, tumeweza kushiriki na kuhamasisha vijana kujiunga katika vikundi vya kujitolea na vya ujasiliamali ambapo mafanikio makubwa yanaonekana katika kikundi cha usafi na uhifadhi wa mazingira mkoa wa Mbeya kiitwacho Umoja wa Vijana Wazalendo Mbeya (UVIWAMBE), ambacho awali walikuwa wanajitolea lakini kwa sasa wananufaika baada ya kupewa kibali cha kukusanya tozo za usafi katika mji mdogo wa Mbalizi, Halmashauri ya wilaya ya Mbeya.

Aidha tunashirikina vema na Halmashauri ya wilaya ya Mbeya katika kujumuika katika ushawishi wa wananchi kuunda vikundi na ushawishi wa kuchangia maendeleo.

Tumeweza kuwachukua na kuwalipia mafunzo ya uchoraji (Artist) watoto na waliokuwa wa mitaani zaidi ya 10 ambao ni chini ya miaka 17 ambao kwa sasa baadhi wanajitegemea na mmoja bado yupo mafunzoni kwa vitendo kupitia mchoraji Asia Print wa Mbeya kwa michango yetu wenyewe kama wanachama.

Kwa sasa tuna vijana wanne wa mitaani ambao tunawalipia mafunzo ya kuendesha pikipiki (Boda Boda) na kila baada ya miezi mitatu tunatembelea hospitali kuona wagonjwa.


MAWASILIANO YA SHIRIKA
Tanzania Community Media Organization (TACOMO).             
S.L.P 705, Mbeya-Tanzania,
SIMU; 0754 440749/0655 440749/0765 615858


Tunaahidi kuwapa ushirikiano mkubwa katika kujuzana taarifa mbalimbali za kimaendeleo.

No comments:

Post a Comment