Shirika letu linaitwa Tanzania Community Media Organization (TACOMO).
TUNAPENDA kutoa shukrani zetu za dhati kwa kutupokea katika njia hii ya mawasiliano kupitia mtandao.
TACOMO PROFILE
JINA KAMILI;
Tanzania
Community Media Organization.
KIFUPI;
Tacomo.
MWANZILISHI NA KIONGOZI MKUU;
Gordon Frank
Kalulunga.
MWAKA WA KUANZA;
2010.
MWAKA WA USAJILI;
Julai 6,
2011.
NAMBA YA USAJILI;
OoNGO/oooo4650
ILIKOSAJILIWA;
Wizara ya
jamii jinsia na watoto.
MAHALA TULIPO;
Mbalizi,
wilaya ya Mbeya (Vijijini) mkoa wa Mbeya.
LENGO NA MADHUMUNI;
Lengo la
shirika ni kusaidia jitihada za serikali katika kuwezesha jamii katika
kuibua na kutatua baadhi ya changamoto za kimaendeleo katika nyanja
mbalimbali zikiwemo za ulinzi wa mtoto, vijana, wazee, jinsia, Afya, Mazingira,
Kilimo na kuandaa warsha/ mafunzo, kushiriki na kushirikishwa katika
shughuli za kimaendeleo na uwezeshaji kwa vikundi
mbalimbali kwa lengo la kutokomeza umasikini.
Aidha
tunashiriki na kushirikishwa katika kuunganisha jamii kwa lengo la kutokomeza
umasikini na kuibua hoja kisha kuifikishia serikali kupitia vyombo vya habari.
KAZI ZA SHIRIKA;
Moja ya kazi
za shirika letu ni kuibua vyanzo vinavyochangia kutokuwa na huduma bora za Afya
ikiwemo matatizo ya wanawake, Ulinzi wa watoto ukatili wa kijinsia na kupatanisha jamii
zilizofarakana.
MAHALI PA KAZI;
Shirika
limesajiliwa kufanya kazi mahala popote Tanzania bara.
MAFANIKIO;
Tangu
shirika letu lisajiliwe kisheria, tumeweza kushiriki na kuhamasisha vijana
kujiunga katika vikundi vya kujitolea na vya ujasiliamali ambapo mafanikio
makubwa yanaonekana katika kikundi cha usafi na uhifadhi wa mazingira mkoa wa
Mbeya kiitwacho Umoja wa Vijana Wazalendo Mbeya (UVIWAMBE), ambacho awali
walikuwa wanajitolea lakini kwa sasa wananufaika baada ya kupewa kibali cha
kukusanya tozo za usafi katika mji mdogo wa Mbalizi, Halmashauri ya wilaya ya
Mbeya.
Aidha tunashirikina
vema na Halmashauri ya wilaya ya Mbeya katika kujumuika katika ushawishi wa
wananchi kuunda vikundi na ushawishi wa kuchangia maendeleo.
Tumeweza
kuwachukua na kuwalipia mafunzo ya uchoraji (Artist) watoto na waliokuwa wa
mitaani zaidi ya 10 ambao ni chini ya miaka 17 ambao kwa sasa baadhi wanajitegemea
na mmoja bado yupo mafunzoni kwa vitendo kupitia mchoraji Asia Print wa Mbeya kwa
michango yetu wenyewe kama wanachama.
Kwa sasa
tuna vijana wanne wa mitaani ambao tunawalipia mafunzo ya kuendesha pikipiki
(Boda Boda) na kila baada ya miezi mitatu tunatembelea hospitali kuona
wagonjwa.
MAWASILIANO YA SHIRIKA
Tanzania
Community Media Organization (TACOMO).
S.L.P 705,
Mbeya-Tanzania,
SIMU; 0754
440749/0655 440749/0765 615858
EMAIL; tacomotz@gmail.com
Tunaahidi kuwapa ushirikiano mkubwa katika kujuzana taarifa mbalimbali za kimaendeleo.
No comments:
Post a Comment