Tuesday 29 March 2016

WANANCHI 78 MBEYA, WAKOSA UMEME TANGU MWAKA 2012

Na Gordon Kalulunga, Mbeya

Wananchi wapatao 78 katika mji mdogo wa Mbalizi jimbo la Mbeya Vijijini mkoani Mbeya, wameshindwa kupatiwa huduma ya umeme tangu walipoomba huduma hiyo mwaka 2012.

Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi alipotembelea katika eneo hilo shina la Umoja Mtakuja, walisema wana uhitaji wa nishati hiyo lakini mpaka sasa wanasubiri majaliwa na matakwa ya shirika la Umeme Tanzania (Tanesco).

Walipoulizwa kama kuna taratibu zozote walizozifanya, walisema tangu mwaka 2012 walijiorodhesha na kupeleka majina yao Tanesco lakini hawajapata jawabu lolote wala kuwaona maafisa wa shirika hilo kupita katika eneo hilo lililopo jirani kabisa na shule ya Sekondari Usongwe ambayo ina umeme.

Mwandishi wa habari hii alifanya jitihada za kuweza kupata majina ya wananchi hao, ambapo alifanikiwa kuyapata majina hayo yakiwa yamesubirishwa katika mafaili ya Tanesco mkoa wa Mbeya.

Majina hayo ni kama yafuatayo;
Boazi Luvanda, Kravery Kazembe, Frank Masinga, John Erasto, Mwanyanje Mwampamba, Issa Mwakifuna, Tosigwe Mwakyusa, Nelbert Mwamwaja, Gimi Ngobile, Ali Ayubu, Maiko Songela, Jasi Mwampashi, Leonard Mwaipopo, Kenneth Simon, Saidi Hayola, Eva Mwakalobo, Pamphili Lema na Paulo Kameta.

Wengine ni Julius Simbeye, Laston Mtafya, Somo Mwakaje, Godwin Sikabenga, Elizabeth Mwalugaja, Waziri Ezekia, Peter Jackson, George mashiwawa, Lazaro Nyusu, Regan Mwankemwa, Gerad Mitingi, William Samson, Geremano Ndelwa, Asajile Godwin, Mlewa Msyani, Aden Kamokene, Mwasomola Mwisivileghe na Tumaini Syonga.

Wananchi wengine waliomo kwenye orodha ya karatasi hiyo ya tangu mwaka 2012 ni Hassan Chaula, Tamali Sampamba, Amani Mwasimba, Felista Josphat, Abdul Ng'elenge, Juma Mwazembe, Aloyce John, Burton Bukuku, Amos Samwel, Tamali Philimon, Gabriel Mtawa, Bahati Ndele na Israel Makobeli.

Wengine ni Maria Mkwela, Gezi Mwashilindi, Jestina Mwalwiji, Hezero Sekeni, Emmanuel Mwandagane, Maiko Yisambi, Justini Francis, Waziri Mwangoka, Luka Kasebele, Edward Mwakyusa, Joseph Kasekwa, Lusajo Boniface na Lusekelo Amenye.

Fadhili Mwashiwawa, Yohana Mbuba, Steven Ngonya, Laison Mwakibinga, Medelina Mwasenga, Mery Pilla, Jackson Halinga, Said Mganga, Sadock Nduka, Sharifu Adson, Mado Godwin, Thobias Mwambona, Paulo Mwewe na Imani Mwaihojo.

Endapo wateja hao wangekubaliwa kupatiwa huduma hiyo ya umeme wa majumbani, kila mmoja angepaswa kulipa kiasi cha Tsh 177,000 ambapo jumla yake ingekuwa Tsh 13,806,000 bila huduma ya nguzo na kila mmoja baada ya kuisha Unit 50 za awali, angepaswa kulipa Tsh. 40,000 ambapo jumla wangelipa 3,120,000 na kila mwezi angelipa Tsh. 10,000 kwa basi shirika hilo lingepata Tsh 780,000 kwa kila mwezi.

No comments:

Post a Comment